Posts

UNAWEZA KUJIAMINI BILA KUONESHA DHARAU?

Image
   Mchezo wa Masumbwi, ni moja kati ya michezo inayotaka kujiamini pasipo kuonyesha dharau ili kuweza kumshinda mpinzani wako Kuna mstari mwembamba sana unaotenganisha maana ya neno kujivuna na kujiamini. Ni vigumu sana kumtofautisha mtu anayejivuna au kwa Kiswahili kingine mtu ‘anayejisikia’ na mtu anayejiamini. Lakini hakuna mtu anayependa kufuatana na mtu anayejisikia, hata watu wanajisikia wanakubali kuwa wanachukia majivuno. Tatizo lililopo katika suala hili ni kwamba watu wengi wanapata tabu sana kutofautisha watu hawa wawili. Mtu anahitaji kujiamini kiasi na siyo kupita kiasi kwa kila jambo. Hivyo mtu anayejiamini ana sifa zipi? Unaweza kumuelezea vipi mtu mwenye majivuno? Na mwisho kabisa, lakini ni muhimu, mtu anaweza je kuwa unajiamini tu bila kujikuta umeingia katika mtego wa watu wenye majivuno? Zijue tofauti hizo: MTU MWENYE MAJIVUNO Mtu mwenye majivuno au anayejisikia, siku zote hujiona ndiye bora. Siku zote hujifanya anajua kitu kilicho bora kwa wengine. Anapofa...

Tunda linavyoweza kukurudisha katika ujana

Image
Tumekuwa tukiulizwa sana swali hili linalohusu matunda. Wasomaji wetu wengi wamekuwa wakitaka kujua namna nzuri ya kula, lakini wengi wakiwa tayari wanajua kwamba matunda na mbogamboga ndiyo vyakula vinavyomfaa zaidi binadamu, wamekuwa wakitaka kujua namna nzuri ya kula matunda. Wengi wetu tunaposikia kula matunda tunadhani ni kuyatafuta au kuyanunua na kuyakatakata halafu kuyatumbukiza mdomoni, kuyatafuna na kuyameza. Hivyo kwa kweli siyo, kwani kuna utaratibu unaofaa wa ulaji wa matunda. Tumeona litakuwa ni jambo la busara iwapo tutakuelezea namna bora ya kula matunda, ili upate faida zaidi ya ulaji huo. Kuna watu wanaokula matunda baada ya chakula. Hili ni kosa kubwa sana. Matunda yanapaswa kuliwa au kunywa kwenye tumbo tupu, yaani wakati mtu akiwa na njaa. Mtu ambaye anaweza kula tunda kwenye tumbo tupu na kabla ya mlo mkuu, anaweza kufaidika zaidi na ulaji huo wa matunda kuliko yule anayefanya kinyume chake. Hebu tuchukulie kwamba ni asubuhi ambapo umekula vipande viwili vya mkate...