Posts

Rahisi kupata na rahisi kukosa!

Kanuni ya kupata unachohitaji maishani ni nguvu iliyopo hapa ulimwenguni kwa ajili ya kuvuta kitu fulani au kulivuta jambo fulani, huzikutanisha nguvu zifanano kwa njia hii ya mvutano. Kanuni hii inajidhihirisha kupitia nguvu ya uumbaji popote pale na kwa namna mbalimbali. Hata kanuni maarufu ya kisayansi ya law of gravity ambayo ndiyo asili ya uundwaji wa ndege ni moja ya kanuni ya kupata unachohitaji maishani. Kanuni ya kupata unachohitaji maishani huvuta mawazo, watu, hali, n.k. Kanuni ya kupata unachohitaji maishani hujidhihirisha katika mawazo yako na kuyavuta na kuyaleta mawazo yanayoshabihiana na mawazo yako; watu wanaofikiri kama wewe, na mambo kama hayo. Kanuni hii ndiyo inayowaunganisha watu wenye mahitaji na utashi unaofanana, ambao wako katika makundi mbalimbali – kama wanasiasa, timu za michezo, wapenzi na mengineyo. Ili kanuni hii iweze kufanya kazi, huhitaji kuwa na uhakika kamili. Kuamua kujenga taswira mawazoni; pia kwa kurudiarudia maneno ya aina fulani mara kwa mara....

UNAWEZA KUJIAMINI BILA KUONESHA DHARAU?

Image
   Mchezo wa Masumbwi, ni moja kati ya michezo inayotaka kujiamini pasipo kuonyesha dharau ili kuweza kumshinda mpinzani wako Kuna mstari mwembamba sana unaotenganisha maana ya neno kujivuna na kujiamini. Ni vigumu sana kumtofautisha mtu anayejivuna au kwa Kiswahili kingine mtu ‘anayejisikia’ na mtu anayejiamini. Lakini hakuna mtu anayependa kufuatana na mtu anayejisikia, hata watu wanajisikia wanakubali kuwa wanachukia majivuno. Tatizo lililopo katika suala hili ni kwamba watu wengi wanapata tabu sana kutofautisha watu hawa wawili. Mtu anahitaji kujiamini kiasi na siyo kupita kiasi kwa kila jambo. Hivyo mtu anayejiamini ana sifa zipi? Unaweza kumuelezea vipi mtu mwenye majivuno? Na mwisho kabisa, lakini ni muhimu, mtu anaweza je kuwa unajiamini tu bila kujikuta umeingia katika mtego wa watu wenye majivuno? Zijue tofauti hizo: MTU MWENYE MAJIVUNO Mtu mwenye majivuno au anayejisikia, siku zote hujiona ndiye bora. Siku zote hujifanya anajua kitu kilicho bora kwa wengine. Anapofa...

Tunda linavyoweza kukurudisha katika ujana

Image
Tumekuwa tukiulizwa sana swali hili linalohusu matunda. Wasomaji wetu wengi wamekuwa wakitaka kujua namna nzuri ya kula, lakini wengi wakiwa tayari wanajua kwamba matunda na mbogamboga ndiyo vyakula vinavyomfaa zaidi binadamu, wamekuwa wakitaka kujua namna nzuri ya kula matunda. Wengi wetu tunaposikia kula matunda tunadhani ni kuyatafuta au kuyanunua na kuyakatakata halafu kuyatumbukiza mdomoni, kuyatafuna na kuyameza. Hivyo kwa kweli siyo, kwani kuna utaratibu unaofaa wa ulaji wa matunda. Tumeona litakuwa ni jambo la busara iwapo tutakuelezea namna bora ya kula matunda, ili upate faida zaidi ya ulaji huo. Kuna watu wanaokula matunda baada ya chakula. Hili ni kosa kubwa sana. Matunda yanapaswa kuliwa au kunywa kwenye tumbo tupu, yaani wakati mtu akiwa na njaa. Mtu ambaye anaweza kula tunda kwenye tumbo tupu na kabla ya mlo mkuu, anaweza kufaidika zaidi na ulaji huo wa matunda kuliko yule anayefanya kinyume chake. Hebu tuchukulie kwamba ni asubuhi ambapo umekula vipande viwili vya mkate...